Social Icons

Wednesday, August 10, 2011

hebu tuangalie kuhusu mapambo ya ukumbi

Jamani kusema ule ukweli mi huwa na admire sana wedding za ki-Naija(Nigeria) hawa watu bwana huwa hawafanyi makosa linapokuja swala la mapambo hasa ya ukumbi na hata wao wenyewe kupangilia mavazi.
Swali ambalo najiuliza kila siku kuhusu wapambaji wetu hapa Bongo hivi hawaoni wenzetu wanavyofanya au???? Hebu tusaidieni kwa kuwa wabunifu mapambo ya ukumbi ni zaidi ya roses na xmas light jamani khaaah!!

Hebu cheki wenzetu walipo .......Nigeria
Ona inavyopendeza

Hizo juu ni taa

Zikiwashwa ndo zawa kama hivi....lovely!!



HAYA HEBU ONA YA KWETU JAMANI....

bongo



hii kidogo afadhali ila nadhani umefika wakati wa kuacha kutumia vitambaa kwa meza ya high table au mnasemaje wadau??

Bado tuna safari ndefu sana kuelekea walipo wenzetu siku hizi hata disco light zinahuu kwenye mapambo ili kufanya mandhali kuwa ya kuvutia kwa rangi tofauti za mwanga wa taa.
Kazi kwenu wataalamu wetu wa mapambo.Najua mnaweza zaidi ya haya kwani hata sasa mnajitahidi.
All the best.

Kisses,
Majoy.

PHOTO CREDITS:Bella Naija(Nigeria) &Adamasgood(TZ)
















No comments:

Post a Comment

Thank you for your comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...